Wednesday, August 16, 2017

MADIWANI SHIRIKIANENI KUIBUA VYANZO VYA MAPATO KATIKA KATA ZENU


pichani ni Mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya ya Hai Mh Helga Mchomvu akizungumza jambo katika kikao cha Baraza la Madiwani Halmashauri ya Wilaya ya Hai na kushoto kwake ni Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya wilaya ya Hai Ndg Yohana Sintoo.

Tuesday, August 15, 2017

ELIMU YA USHIRIKA YASHIKA KASI

Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Ushirika Moshi,Profesa Faustine Karrani Bee akiongea na Wanahabari katika Warsha ya Wanahabari kuhusu Elimu ya Ushirika Nchini na Mchango wa Chuo katika kuendeleza Ushirika.
 
 
baadhi ya wanahabari wakimsikiliza Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Ushirika Moshi,Profesa Faustine Karrani Bee
MOSHI
IMEELEZWA kuwa jitihada za sasa za Serikali kuboresha miundombinu ya usafirishaji  na kupeleka nishati ya umeme vijijini vitapunguza changamoto na kuongeza fursa za viwanda kupitia Ushirika.

Hayo yameelezwa na Makamu Mkuu

Friday, June 9, 2017

MAMIA WAMUAGA NDESAMBURO

Mamia ya waombolezaji wamejitokeza kuaga na kutoa heshima za mwisho kwa aliye wahi kuwa Mbunge wa Moshi Mjini Philemon Ndesamburo,katika ibaada iliyo fanyika leo katika viwanja vya Majengo Moshi,Mkoani Kilimanjaro.

Akitoa salamu za pole Waziri Mkuu Mstaafu na Mjumbe wa kamati kuu ya CHADEMA Taifa Mh Edward Lowassa amesema kuwa  Kila mwanasiasa kutoka katika vyama vya siasa viliyopo hapa nchini anapaswa kufuata mazuri yaliyo fanywa na Ndesamburo ambaye alikuwa chachu ya mabadiliko na maendelo kwa kila kazi aliyo kuwa akifanya.

Amesema kuwa Ndesamburo atakumbukwa kwa mengi mazuri aliyo fanya ambayo yali wafurahisha wanasiasa wote pasipo kujenga chuki hali iliyo pelekea kuwa rafiki wa wanasiasa wote wakongwe na vijana.

Kwa upande wake Askofu wa Kanisa la Ufufuo na uzima Josephat Gwajima amewataka waombolezaji kujenga utamaduni wa kusifia mazuri yanayo fanywa na watu katika jamii angali watu hao wakiwa hai ili waweze kupokea sifa hizo wenyewe jambo litakalo onesha mchango wao moja kwa moja.

Salamu hizo za pole na kuaga mwili wa marehemu umeudhuriwa na  viongozi mbali mbali wa kisiasa,viongozi wa dini ,wageni toka nje ya nchi na wananchi toka kanda mmbali mbali  walio wahi kufanya kazi pamoja na Mzee Ndesamburo.

Mzee Ndesamburo alifikwa na mauti ghafla nyumbani kwake wakati alipo kuwa katika jukumu la kuandika hundi kwaajili ya kutoa rambirambi kwa familia za wanafunzi wa shule ya st vicent Arusha walio pata ajali wakati wakienda masomoni Karatu mei 6 mwaka huu.

Mwili wa Philemon Ndesamburo aliye zaliwa 1935 akiwa na umri wa miaka 82 utazikwa hapo kesho katika makaburi ya nyumbani huko KDC Mbokomu.