pichani ni Mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya ya Hai Mh Helga Mchomvu akizungumza jambo katika kikao cha Baraza la Madiwani Halmashauri ya Wilaya ya Hai na kushoto kwake ni Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya wilaya ya Hai Ndg Yohana Sintoo.
Wednesday, August 16, 2017
Tuesday, August 15, 2017
ELIMU YA USHIRIKA YASHIKA KASI
baadhi ya wanahabari wakimsikiliza Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Ushirika Moshi,Profesa Faustine Karrani Bee
MOSHI
IMEELEZWA
kuwa jitihada za sasa za Serikali kuboresha miundombinu ya usafirishaji na kupeleka nishati ya umeme vijijini
vitapunguza changamoto na kuongeza fursa za viwanda kupitia Ushirika.
Hayo
yameelezwa na Makamu Mkuu
Friday, June 9, 2017
MAMIA WAMUAGA NDESAMBURO
Mamia ya
waombolezaji wamejitokeza kuaga na kutoa heshima za mwisho kwa aliye wahi kuwa
Mbunge wa Moshi Mjini Philemon Ndesamburo,katika ibaada iliyo fanyika leo
katika viwanja vya Majengo Moshi,Mkoani Kilimanjaro.
Akitoa
salamu za pole Waziri Mkuu Mstaafu na Mjumbe wa kamati kuu ya CHADEMA Taifa Mh
Edward Lowassa amesema kuwa Kila
mwanasiasa kutoka katika vyama vya siasa viliyopo hapa nchini anapaswa kufuata
mazuri yaliyo fanywa na Ndesamburo ambaye alikuwa chachu ya mabadiliko na
maendelo kwa kila kazi aliyo kuwa akifanya.
Amesema kuwa
Ndesamburo atakumbukwa kwa mengi mazuri aliyo fanya ambayo yali wafurahisha
wanasiasa wote pasipo kujenga chuki hali iliyo pelekea kuwa rafiki wa wanasiasa
wote wakongwe na vijana.
Kwa upande
wake Askofu wa Kanisa la Ufufuo na uzima Josephat Gwajima amewataka
waombolezaji kujenga utamaduni wa kusifia mazuri yanayo fanywa na watu katika
jamii angali watu hao wakiwa hai ili waweze kupokea sifa hizo wenyewe jambo
litakalo onesha mchango wao moja kwa moja.
Salamu hizo
za pole na kuaga mwili wa marehemu umeudhuriwa na viongozi mbali mbali wa kisiasa,viongozi wa
dini ,wageni toka nje ya nchi na wananchi toka kanda mmbali mbali walio wahi kufanya kazi pamoja na Mzee
Ndesamburo.
Mzee Ndesamburo
alifikwa na mauti ghafla nyumbani kwake wakati alipo kuwa katika jukumu la
kuandika hundi kwaajili ya kutoa rambirambi kwa familia za wanafunzi wa shule
ya st vicent Arusha walio pata ajali wakati wakienda masomoni Karatu mei 6
mwaka huu.
Mwili wa Philemon
Ndesamburo aliye zaliwa 1935 akiwa na umri wa miaka 82 utazikwa hapo kesho
katika makaburi ya nyumbani huko KDC Mbokomu.
Subscribe to:
Posts (Atom)