katika picha ni mkuu wa wilaya ya Hai Anthony Mtaka akipanda miti katika moja kati ya chanzo cha maji kilichopo katika kijiji cha Ng'uni kata ya Masama Kati.
Picha Na Edwine Lamtey 0758-129821
Diwani wa kata ya Masama Kati Deogratius Kimaro akizungumza na wananchi wa kata ya Masama Kati.
Pichani ni mkuu wa wilaya ya Hai Anthony Mtaka mara baada ya kupanda miti.
MKUU wa Wilaya ya Hai Antony Mtaka amewakemea vikali waharibifua wa
mazingira wilayani humo wanao kaidi agizo la kuhifadhi mazingira kwa
kuwachukulia hatua kali za kisheria ili kuhifadhi mazingira.
Mtaka alitoa onyo hilo hapo jana katika
Kata ya Masama Kati kijiji cha Ng’uni alipo kuwa katika uzinduzi wa kampeni ya
upandaji miti ambayo nirafiki wa mazingira
katika vyanzo vya maji vya mto Uwau.
Alisema kuwa suala la utunzaji wa mazingira kwa Mkoa wa
Kilimanjaro kwa baadhi ya maeneo umekuwa
ni wakusuasua huku wananchi wakikaidi sheria za utunzaji wa mazingira zilizo
tungwa katika maeneo yao.
“Itashangaza kwa mtu aliye kufa miaka ya nyuma akifufuka
saivi nakuuangalia Mlima Kilimanjaro kwa theluji yake ilivyo pungua huku misitu
ikiwa imekatwa hovyo na wengine kudirika hadi kulima na kuotesha mazao ndani ya
mito na vyanzo
vyake”Alisema Mtaka.
Mtaka aliwataka Wenyeviti wa
Vijiji katika kata nzima ya Masama Kati
kuwashughulikia wananchi wazembe wanao kaidi sheria za utunzaji wa
mazingira katika ngazi husika au ofisini kwake ili waweze kuchukuliwa adhabu kali na kuwa fundisho kwa wengine
kutokana na viongozi kuchoka na tabia hiyo.
“Hawa watu wanao haribu
mazingira nataka niwa adhibu kwenye haki na sita muonea mtu aibu ambaye
ameshindwa kuyaonea mazingira aibu kwa kuyatunza nita kula nao sahani
moja”.Alisema Mtaka.
Akijibu tuhuma zilizopo za
wananchi wanao lalamikia kutunza miti kasha kukatazwa kuitumia pindi inapo kuwa tayari kuvunwa ili
kujipatia kipato na kulipa ada ya shule,Mtaka alisema kuwa zitpo taratibu
zinazo chukuliwa katika hatua za uvunaji kwa hiyo kinacho takiwa kufanyika ni
kuzuia uvunaji holela na pindi mtu anapo taka kuvuna atatoa taarifa na kuruhusiwa.
“Tuna jua kuwa miti ni sehemu
ya biashara hivyo ni lazima ukate mti kisha upande mti,hivyo unatakiwa
kuangalia jinsi ya kuvuna mti lakini unatakiwa kuwa uwe umesha otesha miti
mingine itakayo kuruhusu kuvuna mti.”Alisema Mtaka
Kwa upande wake Mwenyekiti wa
watumia maji bonde la mto pangani Frank Kimaro alisema kuwa zoezi hilo la
uoteshaji miti lita kuwa ni la muendelezo ambapo mito yote na mifereji ya
watumia maji itatakiwa kupandwa miti rafiki wa mazingira ili kukabiliana na
uharibifu wa mazaingira unao pelekea uwepo wa uhaba wa maji kwa sasa.
Kwa siku ya jana takribani
miti miatano iliwezwa kupandwa katika mto uwau na maeneo mengine ndani ya kata
ya Masama Kati.