Saturday, May 23, 2015

UMEISIKIA HII LAANA?Ireland yaamua kuhusu ndoa za jinsia moja



wapiga kura wajitokeza kwa wingi nchini Ireland ili kuamua kuhusu kuhalalishwa kwa ndoa za watu wa jinsia moja.

Wapiga kura wengi wameripotiwa kujitokeza kwenye kura ya maoni nchini Ireland ya kuamua iwapo ndoa za watu wa jinsia moja zinaweza kuhalalishwa .
Katika sehemu nyingine ukiwemo mji mkuu Dublin na miji mingine, idadi ya wapiga ilitarajiwa kufikia takriban
asilimia 60.

Ndoa za jinsia moja

Wataalamu wengi wa Ireland walio katika mataifa ya kigeni walirudi nyumbani kupiga kura.
Wale wanaounga mkono ndoa za jinsia moja walitarajia watu wengi kujitokeza.

Wapenzi wa jinsia moja wakitoka katika kituo cha kupiga kura

Ikiwa kura hiyo itafanikiwa Ireland itakuwa nchi ya kwanza kuhalalisha ndoa za jinsia moja kupitia upigaji kura.
Matokeo yanatarajiwa kutangazwa baadaye leo.

No comments:

Post a Comment