Mkuu wa Wilaya ya Hai Anton Mtaka aliye shika kichwa akizungumza jambo na OCD | . |
Zaaidi
ya watu 50 hawana makazi wilayani Hai mkoani Kilimanjaro hii ikiwa ni baada ya
mvua iliyonyesha usiku wa kuamkia Jumamosi kuharibu nyumba zao huku pia
mashamba na miundombinu ya barabara, reli nayo ikiharibiwa vibaya.
Wananchi
hao ni katika vijiji vya Rundugai, Mkalama, Chekimaji, Mbatakero na rundugai
ambapo mvua hiyo imeleta madhara kwa baadhi ya kubaki bila makazi huku pia
mifugo ikifa pamoja na uharibifu wa mazao, miundombinu ya barabara na reli
katika maeneo hayo ikiharibiwa vibaya.
“Ilikuwa
ni usiku kama wa saa nane mvua ilipo zidi na maji kuanza kuingia ndani ya
nyumba zetu nilijitahidi kutoka na mke wangu pamoja na watoto wangu kwani hapa
nipo na familia ya watoto kumi kila kitu kimeharibika na sikuweza kutoka hata
na kitu chochote”Alisema mwathirika wa mafuriko hayo.
Kamati
ya maafa wilaya ya Hai ikiongozwa na mkuu waa wilaya ya Hai Antony Mtaka
imetembelea katika maeneo yaliyoathiriwa na mvua hiyo na kujionea hali halisi
huku wakiwapa pole na kuwataka viongozi wa vijiji husika kufanya tathimini
haraka iwezekanavyo ili wananchi hao kuweza kusaidiwa kwa namna yeyote ile.
Mtaka
amesema kuwa maafa yanapotokea hayahitaji siasa na hivyo kuwaomba wale ambao
hawajaathiriwa na maafa hayo kuwapa misaada na hifadhi wale walioathiriwa na
mvua hiyo.
“Niwaombe
wale ambao hawaja kumbwa na mafurikom haya kuwa na utu wa kibinadamu kwa kuwapa
hifadhi wenzao ili kutoa nafasi kwa Serikali kutafuta misaada mingine inayo
hitajika”Alisema Mtaka.
Mtaka
amewaomba kuwa wavumilivu katika kipindi hiki kigumu huku wananchi hao
wakitakiwa kufanya usafi katika maeneo yaliyo athirika ili kuepuka magonjwa ya
milipuko.
“zingatieni
usafi katika maeneo yenu kama mnavyo jua
ya kuwa mvua hiyo imeharibu vyoo vyenu hivyo ni rahisi kwa magonjwa ya mlipuko
kuwapata msipo fanya usafi ikiwa ni pamoja na kulala katika vyandarua katika
hifadhi mtakazo pata”Alisema Mtaka.
Baadhi
wa wanavijiji hao wamedai kuwa tukio kama hilo
liliwahi kutokea mwaka 1965 ambapo lilifanya uharibifu kama
huo huku mashine ya kusaga na kukoboa nafaka wakati huo ikichukuliwa na
maji.”Walisema wanavijiji hao.
Tayari
watu ambao nyumba zao ziliharibiwa na mvua wamekwishapata hifadhi kwa majirani
zao, huku kilio chao kikubwa kikiwa ni chakula na mahitaji mengine muhimu
ambayo ni pamoja na Nguo na wakati huo huo wakiwa hawajui waelekee wapi mara
baada ya kuharibika kwa nyumba zao.
Zifuatazo ni picha katika baadhi ya maeneo yaliyo athiriwa na mafuriko.
No comments:
Post a Comment