Thursday, April 30, 2015

DC HAI “ACHENI KUINGIZA SIASA KATIKA MIRADI YA MAENDELEO”.







kaika picha ni Mkuu wa Wilaya ya Hai Ndg Antony Mtaka akizungumza katika uchaguzi wa wajumbe wa bodi ya maji ya Lyamungo Umbwepicha na Edwine Lamtey 0758129821




myenyekiti mpya wa bodi ya Maji ya Lyamungo Umbwe Michael Sitaki Mmasi


mhandisi wa maji wilaya ya Hai Eng. Nyakaraita Mwita akizungumza na wajumbe wa mkutano wa bodi ya Maji ya Lyamungo Umbwe.

Grace Makiluli katibu tawala msaidizi serikali za mitaa mkoani Kilimanjaro.

HAI

MKUU wa wilaya ya Hai Antony Mtaka amempongeza aliyekuwa Askofu wa KKKT Dayosisi ya Kaskazini Askofu Mstaafu Erasto N kweka  kwa jitihada zake alizozifanya wakati akihudumu kama askofu ikiwamo kupokea miradi mbli mbali ya maji iliyopitia katika Dayosisi Hiyo.

Mtaka ameyasema hayo hii leo wakati wa kikao cha  kumchagua mwenyekiti na wajumbe wa bodi ya maji ya Lyamungo Umbwe kilichofanyika katika shule ya sekondari Lyamungo.

Amesema kuwa ni mfano wa kuigwa kwa kiongozi aliyekuwa mstari wa mbele katika kuiletea jamii maendeleo pasipokuwa na ukiritimba, ubadhirifu na kuweka maslai binafsi ya shughuli za kimaendeleo.

“ ni jambo la bahati sana kwa Askofu Kweka kutanguliza maslai ya Wananchi katika mradi huu wa maji pasipo kujali atanufaika vipi, ingekuwa ni mtu asiyekuwa mwadilifu angegeuza mradi kuwa wake huku wananchi wakiangamia kwa ukosefu wa maji safi na salama.” Alisema Mtaka

“Askofu Kweka alipoke Euro mill. 34 sawa na shilingi Bill. 68 mwaka 1992 ambapo ndipo mradi huo ulianza rasmi ukijumuisha vijiji 11 kutoka Hai na Vijiji 13 kutoka Moshi vijijini, ingekuwa ni mwingine angepeleka wapi?”  Alihoji Mtaka

Sanjari na hayo amewataka viongozi wapya waliochaguliwa kuiongoza bodi hiyo ya Lyamungo Umbwe kuepuka kuchanganya siasa na kazi za miradi ya maendeleo ili miradi hiyo iweze kuwanufaisha wananchi wote na vizazi vya baadae.

“epukeni kutapeliwa na wanasiasa wanaojiingiza katika miradi ya kimaendeleo kwani wengi wao ni wapotoshaji kwa kuingiza siasa katika utendaji” alisema Mtaka.


Kwa upande wake mhandisi wa maji wilaya ya Hai ambaye pia alikuwa msimamizi wa uchaguzi huo Mhandisi Nyakaraita Mwita amewataka wajumbe waliochaguliwa katika bodi hiyo kupeanan ushirikianano katika utendaji ikiwemo pamoja na kushirikiana na halmashauri ili  kuleta ufanisi zaidi.

Ameongeza kuwa jamii inatakiwa kuopata maji safi na salama kama bodi ya maji ilivyojusudia ili kuepuka mnagonjwa mbali mbali yatokanayo na matumizi ya maji yasiyo safi na salama.

Pia amesema kuwa wanawake wamekuwa ni waathirika wakubwa wa utafutaji wa maji safi na salama katika familia zao jambo linalowapelekea kushindwa kushiriki katika  shughuli nyingine za kimaendeleo.

Katika zoezi la upigaji wa kura wajumbe walikuwa 258 ambapo kura moja iliharibika huku Michael Sitaki Mmasy akishikilia nafasi ya mwenyekiti,Emmanuel Izack Show akiwa ni makamu mwenyekiti ambapo walipita bila kupingwa kutokana na kutojitokeza kwa wagombea wengine kuchukua fomu za nafasi hizo kama ilivyotakiwa.


Kwa upande wa wajumbe watendaji wa bodi ya maji, Bibianna Mmasy aliibuka mshindi kwa kupata kura 85 na Bi, Joyce Kweka akipata kura 71 ambazo zote kwa pamoja zilivuka asilimia hamsini iliyoitajika.




Wednesday, April 29, 2015

SITOSUBIRI KUFUKUZWA CHADEMA


Mbunge wa Mpanda Mjini kupitia tiketi ya Chama cha Demkrasia na Maendeleo CHADEMA amesema kuwa hakubaliani na katiba ya chama chake hususani kifungu kinachomzuia mwanachama kwenda mahakamani endapo ataona hajatendewa haki ndani ya chama chake.
Mbunge wa Mpanda Mjini Said Arfi
Mbunge wa Mpanda Mjini kupitia tiketi ya Chama cha Demkrasia na Maendeleo CHADEMA amesema kuwa hakubaliani na katiba ya chama chake hususani kifungu kinachomzuia mwanachama kwenda mahakamani endapo ataona hajatendewa haki ndani ya chama chake.

“Katiba ya CHADEMA naikubali kama katiba ya chama changu, lakini kifungu hicho sikubaliani nacho” aamesema Arfi.
Mbunge huyo pia amesema kuwa hakubaliani na maamuzi ya chama hicho ya kumfukuza uanachama aliyekuwa mbunge wa Kigoma Kaskazini Zitto Kabwe kwa kukiuka kifungu hicho tena bila kufuata utaratibu za vikao.
“Hata kama Zitto alikosea, ilikuwa ni lazima vikao halali vya chama vikae ndiyo viamue, siyo kwa utaratibu uliotumika”
Akizungumzia msimamo wake ndani ya chama hicho, Arfi amesema kuwa yeye bado ni mwanachama hai wa CHADEMA kwa kuwa bado chama hicho hakijamfukuza, na kukiri kuwa aliingia katika mgogoro na viongozi wenzake wakati akiwa Makamu Mwenyekiti wa chama hicho kutokana na kutokubaliana na mwenendo wa baadhi ya viongozi wakuu wa chama hicho.
“Ni kweli tulikuwa na mgogoro uliotokana na mimi kutokubaliana na mwenendo wa viongozi na nikaamua kujiuzulu nafasi yangu, kwa sasa hatuna tatizo tena”
Kuhusu uwezekano wa chama hicho kumfukuza, Arfi amesema kuwa hana tatizo endapo atafukuzwa uanachama, na kwamba hawezi kusubiri kufukuzwa ndani ya chama hicho, isipokuwa “nitatafakari kabla ya kumalizika kwa mkutano wa Bunge na nitafanya maamuzi kama ninatosha kuendelea kuwa CHADEMA, maamuzi yangu nitayatangaza kabla Bunge halijakwisha”
Arfi ametetea uamuzi wake wa kuendelea kubaki ndani ya Bunge Maalum la Katiba na kusema kuwa alikwenda bungeni kuliwakilisha taifa na siyo chama. “Sikwenda katika bunge lile kuiwakilisha CHADEMA”
Amesema msimamo wake ni kuipinga Katiba Inayopendekezwa, kwa kuwa haijajengwa katika misingi ya muundo wa muungano wa serikali tatu.
Kuhusu Uchaguzi ujao, Arfi amesema kuwa bado hajaamua kugombea, lakini kama CHADEMA wakiamua kumfukuza, atawaachia wananchi wa Mpanda wampe muongozo juu ya nini cha kufanya na ni chama gani ataenda kugombea.

Wednesday, April 22, 2015

Mbunge wa Kigoma kusini David Kafulila matatani


Mwanasiasa machachari ambaye pia ni mbunge wa la Kigoma Kusini Mhe. David Kafulila amepandishwa kizimbani katika mahakama ya Wilaya ya Kigoma kujibu shitaka la kumtukana  Mkuu wa Wilaya Uvinza Khadija Nyembo.

Akisomewa mashitaka mbele ya Hakimu David Ngunyale,Wakili wa Serikali Marysinta Lazaro alidai kuwa Kafulila alitenda kosa hilo tarehe 1 mwezi wa 8 mwaka 2013 katika kata ya Nguruka Wilaya ya Uvinza Mkoani kigoma

Wakili Lazaro alidai  kuwa Mbunge huyo alimtolea maneno machafu Mkuu wa Wilaya ya Uvinza kuwa hana maadili,ana akili finyu na ni kiumbe dhaifu kitendo ambacho kingeweza kusababisha uvunjifu wa amani

Upelelezi wa kesi hiyo namba cc6/205 umekamilika na kuomba kupangwa kwa tarehe nyingine kwaajili ya usikilizaji wa awali. Hakimu Ngunyale alikubaliana na ombi hilo la wakili na kuiahirisha kesi hiyo hadi tarehe 19 mei mwaka huu.

Hata hivyo Kafulila alikana shtaka  hilo na kukidhi masharti ya dhamana ambayo ni kuwa na mdhamini mmoja mwenye barua ya utambulisho kutoka ofisi ya mtendaji wa kata na mali isiyohamishika yenye thamani ya shilingi milioni mbili.

Tuesday, April 21, 2015

MADIWANI HAI WACHACHAMAA, WADAI KUMBUKUMBU SAHIHI ZA ARDHI.





Baraza la madiwani wa halmashauri ya wilaya ya Hai limewataka wataalamu wa ardi kutoka nje ya kikao cha baraza hilo na kuleta taarifa sahihi zinazohusiana na ni hekari ngapi ambazo zinamilikiwa na halmashauri katika eneo la mashine Tools na ni majina ya wamiliki yafahamike.

Katika kumbukumbu amabazo zilizowasilishwa katika kikao cha baraza hilo zinaonyesha kuwa halmashauri hiyo inamiliki hekari 17 jambo ambalo lilitolewa maelekezo katika baraza lililopita na kusemekana ni hekari 27 ikiwa na maana kwamba taarifa ilikosewa kuandikwa.

Kati kikao cha leo kwenye kumbukumbu imeonyesha tena ni hekari 17 badala ya 22 ambapo Mh. Rajabu Nkya diwani wa kata ya Machame Mashari amehoji kuwa`` kuna aina fulani ya udanganyifu unaoendelea katika mashamba ya Mashine Tools tunamwomba afisa ardhi atuletee taarisa sahihi kabla ya kumalizika kwa kikao hichi na ikiwa inaonyesha majina ya wamiliki” ``kamati iundwe ili kubaini ukweli na uhalali wa mashamba hayo kwa wamiliki”

Baada ya mvutana wa muda mrefu iliundwa kamati ya watu sita watatu wakiwa ni waheshimiwa madiwani na watatu kutoka katika upande wa wataalam na kupewa wiki mbili katika kushughulikia jambo hilo.

katikati ya watatu waliovaa miwani ni Mbunge Viti maalum Jimbo la Hai Mh. Grace kiwelu akisoma kabrasha la kikao cha madiwani.
picha na Edwine Lamtey 0758-129821

 


mbunge wa Viti maalumu jimbo la Hai Mh. Lucy Owenya akichangia mjadala kuhusiana na hoja ya mapato ya halmashauri 60% kutengwa kwa ajili ya shughuli za kimaendeleo ambapo awali madiwani walitaka kujua ni sababu gani zinakwamisha miradi mingine ya maendeleo katika wilaya kutoendelea hadi sasa
picha na Edwine Lamtey 0758-129821
  
katikati ya picha ni mwenyekiti wa baraza la madiwani Halmashauri ya wilaya ya Hai ndg. Clement   Kwayu, kulia ni makamu mwenyekiti Ally Mwanga na kushoto kwake ni mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya wilaya ya Hai Melkizedeck Humbe
picha na Edwine lamtey 0758-129821


  

Kushoto katika meza kuu ni Mkuu wa wilaya ya Hai Ndg. Antony Mtaka akizungumza katika kikao cha  baraza la madiwani  ikiwa ni mara yake ya kwanza mara baada ya kupata uhamisho toka Mvomero Morogoro kuja Wilaya ya Hai

picha na Edwine lamtey 0758-129821



Monday, April 20, 2015

MAGAZETI APRIL 21 2015










DSC01598





DSC01600



MREMBO MISS BIGSHARK





















MENGI ASHTUSHWA NA HABARI ZA GAZETI

Mwenyekiti mtendaji wa IPP DR. REGINALD MENGI ameeleza kushtushwa na taarifa zilizochapishwa kwenye gazeti la taifa imara zikimtuhumu kuwa ana nia ya kutaka kuiangusha serikali ya Rais Kikwete na kumshughulikia baada ya kumaliza muda wake wa uongozi kunyamaziwa na ikulu na idara ya habari maelezo kwa wiki tatu bila kutoa ufafanuzi wowote.

WATANZANIA WAFANYA VIZURI MBIO ZA NGORONGORO MARATHONI 2015.

WATANZANIA WAFANYA VIZURI MBIO ZA NGORONGORO MARATHONI 2015.

Waziri mkuu Mstaafu ,Fredrick Sumaye akiwa
katika picha ya pamoja na viongozi wengine mbalimbali wakiwemo
waandaji buda mfupi kabla ya kuanza kwa mbio za Km 21 Katika gate la
kuingilia hifadhi ya taifa ya Ngorongoro,
Waziri mkuu Msaatfu Fredirick Sumaye
akikimbia sambamba na rais wa shirikisho la riadha Tanzania,RT,Athony
Mtaka(Kushoto kwake) mkuu wa mkoa wa Arusha ,Daud Ntibenda,pamoja na
mkuu wa wilaya ya Karatau Omary Kwaang kuashiria kuanza kwa mbio za
Ngorongoro Marathoni.

Awawli mbio zikiwa bado ndio zimeanza kundi
la wakimbiaji lilionekana wote wanakimbia kwa karibu.

TANZANIA INAUNGA MKONO TAMKO LA MWENYEKITI WA AU NA SADC MZEE ROBERT MUGABE KUHUSU MACHAFUKO YA AFRIKA KUSINI

TANZANIA INAUNGA MKONO TAMKO LA MWENYEKITI WA AU NA SADC MZEE ROBERT MUGABE KUHUSU MACHAFUKO YA AFRIKA KUSINI

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Mh. Bernald Membe akizungumza na waandishi wa habari kwenye ukumbi wa JNICC jijini Dar es salaam, Wakati alipotoa tamko la serikali ya Tanzania kuhusu machafuko yaliyotokea wiki iliyopita nchini Afrika Kusini kwa wenyeji wa nchi hiyo kufanya mashabulizi dhidi ya wageni kutoka mataifa mbalimbali ya Afrika wanaoishi nchini humo.
Amesema kuna habari zimeenea kwenye mitandao mbalimbali kuwa kuna watanzania wamekufa, Ni kweli ila watanzania hao wamekufa katika matukio tofauti na vurugu hizo amesema watanzania waliokufa katika matukio hayo ni Athman China alipigwa kisu gerezani  , Rashid Mohamed aliyeuwawa kilomita 90 kwa tukio la uporaji na Ali Heshi Mohamed aliyekufa kwa  ugonjwa wa TB kutokana na maelezo ya Polisi wa nchini humo.
    
Baadhi ya wanahabari wakiwajibika. 6