IMEELEZWA
kuwa hali ya ubadhirifu wa mali ya umma kwa baadhi ya viongozi wilayani hai
mkoani Kilimanjaro imesababisha jamii kuto kufikia malengo ya kimaendeleo kwa
wakati.
Hayo
yamesemwa na mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya ya hai Clemence Kwayu wakati
wa kikao cha baraza la madiwani leo huku
akikemea suala hilo kwani limekuwa likiibua migogoro baina ya wananchi na viongozi.
Pia
amesema kuwa kila kiongozi atakaye tuhumiwa kwa kosa la ubadhirifu wa mali ya
umma atachukuliwa hatua kali za kisheria kwa mapema ili kuwa mfano na fundisjho
kwa viongozi wengine wenyetabia kama hiyo.
Kwayu
amesisitiza kwa kusema kuwa ni wajibu kwa kila kiongozi kufuata sharia na
kanuni za uongozi,kujenga tabia ya kuhifadhi kumbukumbu pindi wanapo chukua
michango toka kwa wananchi.
Kwa
upande wake mkurugenzi wa halmashauri Melkzedeck Humbe amewashauri madiwani kuepuka usimamizi
mbovu wa fendha na mali za umma kwa maslahi binafi na kuwakumbusha kuwa
kiongozi ni zaidi ya kioo kwa jamii.
No comments:
Post a Comment