TANZANIA INAUNGA MKONO TAMKO LA MWENYEKITI WA AU NA SADC MZEE ROBERT MUGABE KUHUSU MACHAFUKO YA AFRIKA KUSINI
Waziri
wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Mh. Bernald Membe
akizungumza na waandishi wa habari kwenye ukumbi wa JNICC jijini Dar es
salaam, Wakati alipotoa tamko la serikali ya Tanzania kuhusu machafuko
yaliyotokea wiki iliyopita nchini Afrika Kusini kwa wenyeji wa nchi hiyo
kufanya mashabulizi dhidi ya wageni kutoka mataifa mbalimbali ya Afrika
wanaoishi nchini humo.
Amesema
kuna habari zimeenea kwenye mitandao mbalimbali kuwa kuna watanzania
wamekufa, Ni kweli ila watanzania hao wamekufa katika matukio tofauti na
vurugu hizo amesema watanzania waliokufa katika matukio hayo ni Athman
China alipigwa kisu gerezani , Rashid Mohamed aliyeuwawa kilomita 90
kwa tukio la uporaji na Ali Heshi Mohamed aliyekufa kwa ugonjwa wa TB
kutokana na maelezo ya Polisi wa nchini humo.
Wapiga
picha kutoka vyombo mbalimbali vya habari wakichukua picha na taarifa
muhimu wakati Waziri huyo akizungumuza na waandishi wa habari kwenye
ukumbi wa JNICC jijini Dar es salaam asubuhi hii. Baadhi
ya waandishi wa habari wakifuatilia kwa makini wakati Waziri wa Mambo
ya Nje na Ushirikini wa Kimataifa akizungumza na waandishi wa habari
jijini Dar es salaam.
Balozi wa Tanzania Umoja wa Mataifa Mh ModestJ Mero pamoja na viongozi
wengine kutoka wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa
wakifuatilia mkutano huo.
No comments:
Post a Comment