Thursday, August 6, 2015

TAHARUKI YATANDA KWA WAKULIMA



katika picha ni baadhi ya mifugo iliyokamatwa katika kijiji cha  Mungushi  kitongoji cha Nkwamakuu mara baada ya wafugaji kutoka maeneo ya Longido, siha na Kiteto kudaiwa kuvamia mashamba ya wakulima na kuanza kulishia.Picha na Edwine Lamtey 0758129821




Kundi la mifugo lililokamatwa na kufikiswa katika eneo la Halmashauri ya wilaya ya Hai.

baadi ya watuhumiwa wanaodaiwa kuingiza mifugo yao katika mashamba ya wakulima.




Zaidi ya mifugo wapataoelfu tano (5,000) wanasadikiwa kuingia katika kijiji cha Mungushi na kuharibu mazao ya wakulima ambapo hadi sasa haijafahamika idadi kamili ya uharibifu huo huku mabishano makali yakitokea baina ya Polisi na wafugaji.

Akizungumza na Bomanews mwenyekiti wa kijiji cha Mungushi Simbo Eben Mbasha amesema kuwa kuanzia Agost 1 mwaka huu wamekuwa wakishuhudia makundi mbali mbali ya mifugo kutoka wilaya jirani za Siha,Simanjiro na Kiteto ambapo wamekuwa wakichungia mifugo hiyo katika mashamba ya wakulima.

Bomanews imeshuhudia kundi la mifugo zaidi ya 280 waliokamatwa huku pia watu watano wakishikiliwa na jeshi la polisi kwa uvamizi huo.

Hata hivyo kwamujibu wa mwenyekiti wa kijiji hicho bado ulinzi na usalama umeimarishwa katika maeneo hayo na wananchi wakiaswa kutoa taarifa endapo wataona dalili zozote za uvunjifu wa amani.

Friday, July 31, 2015

MAKAMU WA RAIS DKT. BILAL AWEKA JIWE LA MSINGI UJENZI WA BARABARA YA KIA-MERERANI, JIJINI ARUSHA.

ma1
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akihutubia wananchi wa Mji mdogo wa Mererani, wakati wa hafla ya kuweka Jiwe la Msingi la Ujenzi wa Barabara ya Kia-Mererani yenye Kilometa 26. Hafla hiyo imefanyika leo Julai 30, 2015. Picha na OMR
ma2
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Mohammed Gharib Bilal, Waziri wa Ujenzi, Dkt. John Pombe Magufuli, na baadhi ya viongozi wakifunua kitambaa kwa pamoja kuashiria kuweka Jiwe la Msingi la Ujenzi wa Barabara ya Kia-Mererani, wakati wa hafla fupi iliyofanyika mji mdogo wa Mererani, leo Julai 30, 2015. Picha na OMR
ma3
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Mohammed Gharib Bilal, Waziri wa Ujenzi, Dkt. John Pombe Magufuli, na baadhi ya viongozi wakifunua kitambaa kwa pamoja kuashiria kuweka Jiwe la Msingi la Ujenzi wa Barabara ya Kia-Mererani, wakati wa hafla fupi iliyofanyika mji mdogo wa Mererani, leo Julai 30, 2015. Picha na OMR
ma4
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, Waziri wa Ujenzi, Dkt. John Pombe Magufuli na baadhi ya Viongozi,kwa pamoja wakikata utepe kuashiria kuzindua rasmi harakati za ujenzi wa Barabara ya Kilometa 26 ya Kia-Mererani, wakati wa hafla hiyo iliyofanyika mji mdogo wa Mererani leo Julai 30, 2015. Picha na OMR
ma5
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akivishwa vazi la kabila la Masai na Kiongozi wa Mila ya Laibuwanani, Kisota Lengitambi, wakati wa hafla hiyo ya uwekaji wa Jiwela Msingi la Ujenzi wa Barabara ya Kia-Mererani. leo julai 30, 2015. Picha na OMR
ma6
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya viongozi wa makabila mawili makubwa ya Kimasai baada ya kumvisha vazi hilo. Picha na OMR
ma7
Dkt. Bilal akiagana na viongozi hao wa kabila la Masai.
ma9
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akipanda mti wa kumbukumbu  baada ya kuweka Jiwe la Msingi la Ujenzi wa Barabara ya Kia- Mererani, leo Julai 30, 2015. Picha na OMR
ma10
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya viongozi. Picha na OMR
ma11
Waziri wa Ujenzi, Dkt. John Magufuli, akizungumza kabla ya kumkaribisha Mgeni rasmi, Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal. Picha na OMR
 ma13
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, Waziri wa Ujenzi, Dkt. John Magufuli, wakicheza sambamba na kinamama wa kabila la Kimasai wakati wakifurahia ngoma ya Kimasai kwenye hafla ya uwekaji wa Jiwe la Msingi la Ujenzi wa Barabara ya Kia-Mererani, leo Mkoani Manyara. Picha na OMR
ma14
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, Waziri wa Ujenzi, Dkt. John Magufuli, wakifurahia ngoma ya asili kwenye hafla ya uwekaji wa Jiwe la Msingi la Ujenzi wa Barabara ya Kia-Mererani, leo Mkoani Manyara. 

EDWARD LOWASSA ACHUKUA FOMU ZA KUGOMBEA URAIS KUPITIA CHADEMA

unnamed (5)

WAZIRI Mkuu wa zamani Edward Lowassa, amechukua fomu kupeperusha bendera ya  Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kimpitishe kugombea urais kupitia Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa) ifikapo Oktoba 25 mwaka huu.

Katika Makao Makuu ya chama chake hicho kipya leo Edward  Lowassa alipokewa na maelfu ya watu waliovalia sare za chama huku wakiimba wana imani naye.

Edward Lowassa aliwasili makao makuu mchana moja kwa moja akaenda ofisi za Katibu Mkuu Dk. Wilbroad Slaa.
Huku akisindikizwa na Mwenyekiti Freeman Mbowe, Mwanasheria wa chama Tundu Lissu na Naibu Katibu Mkuu Zanzibar Salum Mwalimu, Edward Lowassa aliingia katika  ofisi hizo katika jukwaa maalumu la kupokea fomu.
Lissu ndiye alikuwa mzungumzaji wa kwanza kwa kuwahakikishia wanachama hawakubahatisha kumpokea Lowassa kwa sababu walifanya utafiti wa kina.

“Kamati Kuu imejiridhisha kwa kushirikiana na viongozi wote wa juu akiwemo Katibu Mkuu na manaibu wake wote wawili, Mwenyekiti na makamu wote wawili, wajumbe wa Kamati Kuu na Mkutano Mkuu, kuwa Edward Lowassa ndiye kiongozi tunayemtaka hivyo Jumapili iliyopita tuliitisha Kamati Kuu ya dharura kumpitisha,” alisema Lissu.
Baada ya kukabidhiwa fomu aliyolipiwa na wanachama waliochangishana fedha  hadi kufikia Sh milioni moja, Edward Lowassa alisimama kuwasalimia waliohudhuria kwa kuwaahidi kufanya kazi kwa juhudi ili kuiondoa Tanzania katika hali mbaya ya kiuchumi.

“Nashukuru kwa kunipa heshima kubwa namna hii, sina maneno ya kuwashukuru zaidi ya kuahidi kufanya kazi kwa bidii ili iwe malipo ya mlichonifanyia.

“Shukurani yangu itakuja baada ya kushinda uchaguzi, lakini ushindi hauji bila umoja. Chadema inaweza kuleta mabadiliko kupitia ukawa.

Baada ya kumaliza kuzungumza alisimama Mbowe kutoa neno la shukurani kwa Edward Lowassa kwa kusema Chadema kitaendelea kuwa chama makini kinachosimamia maamuzi yake.

Vilevile alizungumzia ratiba ya vikao vya kujadili fomu ya mgombea ambaye mpaka sasa ni Edward Lowassa pekee, “Vikao vitaanza Agosti mbili kujadili namna tutakavyoingia katika uchaguzi mkuu.

“Baraza Kuu litaketi Agosti tatu kujadili fomu ya mgombea na kujadili ilani ya uchaguzi, Mkutano Mkuu utafanyika Agosti nne kupitisha jina la mgombea na mgombea mwenza.

“Vikao vya kamati  Kuu vitaendelea tarehe tano, sita hadi saba kuidhinisha wagombea wa ubunge kwa kushirikiana na Ukawa. Kazi ya kujadili wagombea si ndogo nawaomba waandishi wa habari muwe wavumilivu msipige ramli,” alisema Mbowe.

Baada ya kumalizika hafla hiyo Edward Lowassa alitoka nje kwa ajili ya picha ya pamoja kuwaonyesha wanachama fomu yake.

Tuesday, July 28, 2015

Madereva wengi nchini hutelekezwa na wamiliki wa magari


Madereva wengi nchini hutelekezwa na wamiliki wa magari bila kuwapatia huduma ya matibabu punde wanapopatwa na ajali au kuugua wakiwa kazini, kutokana na wamiliki hao kukwepa kuwagharimia huduma za matibabu.

Tuesday, June 9, 2015

ZOEZI LA UANDIKISHWAJI KWA MFUMO WA BVR LASITISHWA


 Katika picha ni washirikiwa wa mafunzo ya BVR wilayani Hai mkoani Kilimanjaro wakipokea mafunzo na matumizi ya mashine za BVR ili kuandikisha wapiga kura katika daftari la kudumu.



katika picha ni Murugenzi Mtendaji wa halmashauri ya wilaya ya Hai Said Ahamed Said Mderu akizungumza na waandikishaji wasaidizi na BVR Operator huku pia akitoa taarifa ya kusogezwa mbele kwa zoezi hilo.





 katikati ni mkuu wa wilaya ya Hai ndg. Anthony Mtaka mara baada ya kuzungumza na washiriki wa mafunzo ya BVR kulia ni mkurugenzi mtendaji wa Hai ndg. Said Mderu na kushoto kwake ni mkuu wa kitengo cha uchaguzi/msimamizi ngazi ya wilaya ndg. Edward Ntakirio

Picha Na:
Edwine Lamtey

Friday, June 5, 2015

DC HAI: ATAKAYEFANYA UZEMBE UANDIKISHAJI KUKIONA CHA MTEMA KUNI

Zoezi la uandikishaji wa wapigaji kura katika daftari la kudumu la wapigaji kura unatarajia kuanza tarehe 9 mwezi huu wilayani Hai mkoani Kilimanjaro huku wanachi wakiaswa kujitokeza kwa wingi kushiriki katika zoezi hilo.

Akifungua mafunzo kwa waandikishaji wa daftari la kudumu kwa wapiga kura mkuu wa wilaya ya Hai Anthony Mtaka amesema kuwa kazi ya uandikishaji inahitaji ueledi wa hali ya juu pamoja na uaminifu  ili kuleta tija na mafanikio

Wednesday, June 3, 2015

TIMU YA ULINZI KWA MTOTO HAI MFANO WA KUIGWA


 mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya ya Hai Clementi Kwayu akizungumza na wajumbe wa kamati ya ulinzi kwa mtoto ngazi ya wilaya. Picha na Edwine Lamtey 0758-129821






mwenyekiti wa timu ya Ulinzi kwa mtoto Bi. Helga akiwasilisha moja kati ya Taarifa kwa wajumbe wa timu ya ulinzai kwa mtoto.






wajumbe wa timu ya ulinzi kwa mtoto wakimsikiliza mwenyekiti wa timu hiyo Bi. Helga
Picha zote Na, Edwine Lamtey



AWATAPELI WAFANYABIASHARA,DC AMSOTA RUMANDE, ADAI AMETOKA OFISI YA WAZIRI MKUU.


Aliyesimama ni mtuhumiwa Praygod Mmasy anayedaiwa kuwatapeli wamiliki wa Sheli, pamoja na viwanda kwa kujifanya mtumishi kutoka ofisi ya waziri mkuu kitengo cha mazingira.  Picha na Edwine Lamtey



 kulia katika picha ni mmiliki wa kiwanda cha Harso mara baada ya kutapeliwa kiasi cha sh.1,500,000 Katikati ni mtuhumiwa Praygod Mmasy na mwisho kushoto ni mkuu wa idara ya mazingira mkoani Kilimanjaro.



kushoto ni mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya ya Hai Clement Kwayu katikati ni OCS wa kituo cha polisi Bomang'ombe akifuatiwa na afisaa wa Takukuru bwana Fidelis Maparara





katika picha ni mkuu wa wilaya ya Hai Anthony Mtaka akizungumza kuhusiana na tukio hilo la kutapeliwa kwa wafanyabiashara kikao ambacho kilijumuisha Kamati ya ulinzi na usalama, wafanyabiashara waliotapeliwa pamoja na waandishi wa Habari.

WALIOTAPELIWA
Limcolim M.Lema sh.1,000,000/=
Nicky Munuo sh.3,500,000/=
A. Salakana sh. 200,000/=
H. A. Shoo sh. 1,500,000/=

Monday, June 1, 2015

UWT HAI YASAIDIA WAHANGA WA MAFURIKO MIJONGWENI.








baadhi ya wahanga wa mafuriko Mijongweni wakipokea msaada toka UWT




Katika picha kushoto ni diwani wa viti maalu Bi. Hausen Nkya akiwa na mjumbe UWT wakati wa kukabidhi msaada huo.
picha na Edwine Lamtey



Diwani wa kata ya Longoi Nasibu Mndeme akipokea msaada uliotolewa na UWT
Umoja wa wanaaake wa chama cha mapinduzi UWT wilayani Hai mkoani kilimanjaro umekabidhi vitu mbalimbali kwa waathirika wa mafuriko ya mvua yaliyotokea mwanzoni mwa mwezi May mwaka huu.
Akipokea msaada huo diwani wa kata ya Machame Kusini Nasibu Mndeme amesema kuwa anaushukuru umoja huo kwa msaada walioutoa kwa walengwa na kuahidi kuwa watapatiwa walengwa kama ilivyokusudiwa.

Saturday, May 30, 2015

ARUSHA YAFURIKA, BARABARA KUFUNGWA KWA MASAA KADHAA


Baada ya kusubiri sana. Leo ndio ile siku tunaianza rasmi safari ya Matumaini hapa uwanja wa Sheikh Amri Abeid Arusha. Karibu ujiunge nasi. Kama hutaweza kufika unaweza kutazama mkutano LIVE ONLINE. Bofya hapa bit.ly/1LQfLQ3.
Pia mkutano huu utaonyeshwa LIVE na ITV, EATV (Channel 5), Clouds TV na Channel Ten. USIKOSE

Wednesday, May 27, 2015

YANGA NDIYO WALIOMWAGA FEDHA NYINGI ZA USAJILI HADI SASA



Wakati harakati za usajili zinazidi kupamba moto, mabingwa wa Tanzania Bara, Yanga wanaonekana kuwa ndiyo waliomwaga fedha nyingi zaidi katika kipindi cha usajili.


Yanga wamemwaga zaidi ya Sh milioni 195 katika fedha zao ambazo wametumia kwa ajili ya kuimarisha kikosi chao na watamwaga zaidi ya hizo hadi watakapokuwa wamemaliza.

Gharama zinaweza kufikia zaidi ya Sh milioni 200 hadi sasa kama itajumlishwa na fedha walizowatumia wachezaji kwa ajili ya usafiri kutoka katika miji ya Mbeya, Zanzibar na pia kuwasafirisha wengine.

Wako ambao waliboresha mikataba yao na wengine wapya ambao tayari wameishatua Jangwani kwa ajili ya msimu ujao.

Kwa upande wa Simba, nao wanaonekana kujitutumua kwani katika fedha kwa ajili ya kuimarisha kikosi chao ukianzia zile za Jonas Mkude hadi sasa, tayari wametoa zaidi ya Sh milioni 165.

Simba wameboresha baadhi ya mikataba ya wachezaji wao lakini inaonekana pia bado wanaweza kufikia Sh milioni 200 na zaidi kwa kuwa bado wanahitaji kuboresha mkataba wa Ramadhani Singano ‘Messi’, Ivo Mapunda na pia kusajili wachezaji wapya.

Yanga (Sh milioni 195):
Deus Kaseke kutoka Mbeya City (Sh milioni 35), Haruna Niyonzima (Sh milioni 70), Mbuyu Twite (Sh milioni 30), Deogratius Munish ‘Dida’ (Sh milioni 20) na Benedict Tinocco kutoka Kagera (Sh milioni 20) na Haji Mwinyi Mgwali kutoka KMKM (Sh milioni 20).

Simba (Sh milioni 165):
Jonas Mkude (Sh milioni 60), Said Ndemla (Sh milioni 30), Hassan Isihaka (Sh milioni 30), Paul Mwalyanzi kutoka Mbeya City (Sh milioni 25), William Lucian ‘Gallas (Sh milioni 20).