Friday, June 5, 2015

DC HAI: ATAKAYEFANYA UZEMBE UANDIKISHAJI KUKIONA CHA MTEMA KUNI

Zoezi la uandikishaji wa wapigaji kura katika daftari la kudumu la wapigaji kura unatarajia kuanza tarehe 9 mwezi huu wilayani Hai mkoani Kilimanjaro huku wanachi wakiaswa kujitokeza kwa wingi kushiriki katika zoezi hilo.

Akifungua mafunzo kwa waandikishaji wa daftari la kudumu kwa wapiga kura mkuu wa wilaya ya Hai Anthony Mtaka amesema kuwa kazi ya uandikishaji inahitaji ueledi wa hali ya juu pamoja na uaminifu  ili kuleta tija na mafanikio
katika mchakato mzima.

Aidha Mtaka amesema kuwa serkali  haitowavumilia wale wote ambao watakwamisha zoezi hilo na wale wote watakaopewa dhamana ya kuendesha zoezi hilo watambue kuwa ni zoezi nyeti na lenye maslai ya taifa na wananchi kwa ujumla.

Awali akimkaribisha mkuu wa wilaya, mkurugezi mtendaji wa halmashauri  ya wilaya ya Hai Said  Ahamed Said Mderu amesema kuwa halmashauri tayari imekwishapokea mashine 50 za BVR katika uendeshaji wa zoezi hilo huku akibainisha kuwa wilaya ilihitaji mashine 44 na hivyo kuna ongezeko la mashine 6 na kuifanya halmashauri kuwa na uhakika wa kukamilisha zoezi hilo kwa ufanisi mkubwa.

zoezi la uandikishaji wa wapigaji kura katika daftari la kudumu linatarajia kuendeshwa kwa siku 28 wilayani Hai kuanzia Juni 6 hadi julai 04 mwaka huu

Zoezi la uandikishaji wa wapiga ura  katika dftari la kudumu linatarajia kuanza rasmi wiki ijayo tarehe 9 ya mwezi huu wilayani Hai mkoani Kilimanjaro ambapo wananchi wameaswa kujitokeza kwa wingi kushiriki katika zoezi hilo.

Akizungumza na Bomanews.blogspot.com   mkurugenzi mtendaji wa wilaya ya Hai Said Ahamed Said Mderu amesema kuwa tayari halmashauri imekwishapokea vifaa vya kuendeshea zoezi hilo ambapo wilaya ina mashine 50 huku itaji lilikuwa ni mashine 44 na kubainisha kuwa kuna ongezeko la mashine 6 ambazo zitasaidia kuleta ufanisi zaidi.

Zoezi hili linatarajiwa kuanza juni 9 na kumalizika julai 4 mwaka huu na uandikishwaji utafanyika katika vijiji vyote wilayani hapo katika maeneo ambayo yatakuwa yametengwa kwa ajili ya zoezi hilo.



No comments:

Post a Comment