Saturday, May 16, 2015

TUSAIDIE WAHANGA WA MAFURIKO


Aliyevalia shati jeupe ni Mkuu wa Wilaya ya Hai Ndg Anthony Mtakakushoto kwake ni Mbunge wa jimbo la Hai Freeman Mbowe, anayemfuata ni mbunge wa viti maalumu Lucy Owenye na kulia ni Meneja Nmb kanda ya Kaskazini Bi. Vicky Bishobe wakikabidhi misaada kwa wahanga wa mafuriko
 picha na Edwine Lamtey







meneja Nmb Kanda ya Kaskazini akimkabidhi mkuu wa wilaya ya Hai vitu vilivyotolewa na Benki hiyo.

katibu tawala wa Wilaya ya Hai Bi. Chikira akionyesha fedha alizopoke kutoka kwa mbunge mara baada ya kukabidhiwa.









Imeelezwa kuwa bado wadau mbali mbali  wanahitajika kujitokeza na kuendelea kusaidia waathirika wa mafuriko ya mvua iliyoleta maafa katika kata ya weru weru na masama rundugai.

Hayo yamesemwa na mkurugenzi wa Wilaya ya Hai ndg. Said Ahamed Mderu wakati akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake.

Mderu amesema kuwa mbali na misaada iliyotolewa na NMB,Mbunge Mbowe na wadau wengine bado mahitaji zaidi yanahitajika ili waathirika kurejea katika maisha yao ya kawaida.

Ikumbukwe hivi karibuni Banki ya Nmb ilitoa msaada wa vitu mbali mbali venye jumla ya sh. mil. 10 kupiti meneja wa Kanda ya Kaskazini Bi. Vicky Bishobe huku pia mbunge wa jimbo la Hai Freeman Mbowe akitoa fedha taslimu zaidi ya mil. 5 na pia kuchangia sh. mil. 1.5 kwaajili ya ujenzi wa choo cha shule ya Elerai

No comments:

Post a Comment