Tuesday, August 15, 2017

ELIMU YA USHIRIKA YASHIKA KASI

Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Ushirika Moshi,Profesa Faustine Karrani Bee akiongea na Wanahabari katika Warsha ya Wanahabari kuhusu Elimu ya Ushirika Nchini na Mchango wa Chuo katika kuendeleza Ushirika.
 
 
baadhi ya wanahabari wakimsikiliza Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Ushirika Moshi,Profesa Faustine Karrani Bee
MOSHI
IMEELEZWA kuwa jitihada za sasa za Serikali kuboresha miundombinu ya usafirishaji  na kupeleka nishati ya umeme vijijini vitapunguza changamoto na kuongeza fursa za viwanda kupitia Ushirika.

Hayo yameelezwa na Makamu Mkuu
wa Chuo Kikuu cha Ushirika Profesa Faustine Karrani Bee katika ufunguzi wa warsha ya Chuo Kikuu cha Ushirika Moshi na Wanahabari kuhusu elimu ya Ushirika Nchini na mchango wa Chuo katika kuendeleza ushirika Prof. Faustine Bee amesema kuwa

Ushirika ndio njia pekee ya usawa ya kujenga uchumi utakao milikiwa na watanzania ambapo uchumi utamuondoa Mtanzania katika umaskini na kumuwezesha kumiliki rasilimali za nchi.

Bee amesema kuwa Tafiti,elimu na ushauri vinavyotolewa na chuo cha Ushirika Moshi vinahitaji na vimekuwa vikipata ushirikiano wa karibu kutoka kwa wanahabari ili kufikia malengo yanayo tarajiwa ya jamii kuwa na uelewa na kuzidi kuviamini vyama vya ushirika nchini.

Chuo kikuu cha Ushirika kitazamia mtazamo chanya kwa watanzania katika kufikia malengo ya ushirika hapa nchini,kwa kushirikisha wadau mbalimbali katika kutoa elimu ya Ushirika na kuhakikisha kuwa jamii inapata habari sahihi za Ushirika.

Ameongeza kuwa kwa sasa vyama vingi vya ushirika vimekuwa na changamoto mbalimbali zilizo pelekea uaminifu wa vyama vya ushirika kutoweka katika jamii,hivyo kumtaka Mrajisi wa vyama vya Ushirika kufanya jitihada za kurudisha imani hiyo kwa wananchi kwa kutoa maelekezo kwa vyama vya msingi vya ushirika nchini.

Kwa upande wa Wanahabari katika Warsha hiyo wametaka Chuo kikuu cha Ushirika ambacho ndio watendaji  wakuu wa Elimu ya Ushirika nchini kuondoa dhana ya kupenda kuongelewa kwa mazuri kwani wengi hawapendi kukosolewa na ndio chanzo cha kuwa mbali na wanahabari.

Aidha wamebainisha kuwa vyombo vya habari vimekuwa vikishutumiwa kwamba vinaleta uchochezi pale vinapo tafuta na kutoa taarifa kuhusu ubadhirifu na madhaifu mengine ya ushirika jambo ambalo ni kinyume  hivyo kutaka Chuo hicho kutoa elimu kwa jamii na watendaji wa bodi za vyama vya ushirika kukubali kazi za wanahabari.

Warsha hiyo imelenga kuanzisha na kuendeleza ushirikiano wa pamoja kati ya chuo kikuu cha Ushirika Moshi- MOCU na Wanahabari katika kutekeleza mpango wa kuendeleza Elimu ya Ushirika hapa nchini pamoja na kutoa fursa kwa wanahabari kufahamu shughuli mbalimbali zinazofanywa na chuo katika kutoa elimu ya ushirika.

No comments:

Post a Comment